Peter Kenneth

IMEBAKIA wiki moja kufanyika Uchaguzi Mkuu nchini Kenya ambapo, tayari wagombea wanane wameshapitishwa na  Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).
Mohamedi Abduba Dida
Miongoni mwa wagombea urais ni pamoja na Mohamedi Abduba Dida alizaliwa mwaka 1975 katika Wilaya ya Wajir. Dida, aliyekuwa mwalimu, anagombea urais kupitia Muungano wa  Mabadiliko Halisi (Alliance for Real Change). Mgombea mweza wake ni Joshua Odongo Onono, ambaye pia alikuwa mwalimu.
Dida, Alisema elimu inapaswa kuwa bure kwa Wakenya wote, na siyo kwa kutegemea mfumo wa ruzuku. Ana digrii ya elimu kutoka chuo kikuu cha Kenyatta na kwa sasa anafanya shahada ya uzamili katika masomo ya dini kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.

Dida amefundisha katika shule kadhaa, ikiwa ni pamoja na kufundisha fasihi ya Kiingereza na dini katika Shule ya Sekondari ya Daadab katika kambi mchanganyiko ya wakimbizi na baadaye katika Shule ya Lenana.
Martha Wangari Karua
Mgombea pekee mwanamke, Martha Karua katika kinyang’anyiro cha urais, alizaliwa Septemba 1957 huko Kirinyaga, Jimbo la Kati.
Karua, mbunge wa Gichugu, anagombea kupitia National Rainbow Coalition pamoja na aliyekuwa mjumbe wa Baraza la Bunge la Afrika Mashariki Augustine Lotodo.
Karua ameapa kuwakilisha Muungano wa Kenya pamoja na jukwaa la mabadiliko ya uchumi na jamii, ikiwa ni pamoja na huduma za afya kila mahali na kuifanya Kenya kuwa kitovu cha uchumi katika kanda.
Alisema atatoa asilimia 10 ya bajeti ya Kenya kuboresha uzalishaji wa kilimo, kuongeza vyanzo vya nishati rejezi na kufanya kazi kuwa ili kuwezesha upatikananji wa intaneti kwa asilimia 50 kwa Wakenya katika miaka mitano.  Karua ana shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na shahada ya uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Marekani, Nairobi.
Kuanzia mwaka 1981 hadi 1987, Karua alifanya kazi mahakamani, alipanda kutoka hakimu wa wilaya hadi hakimu mkuu mkazi. Baada ya hapo amekuwa na shirika la uwakili binafsi hadi 2002. Mwaka 1992, Karua alichaguliwa kuwa mbunge wa Gichugu, kiti ambacho anakishikilia hadi sasa.
Peter Kenneth
Peter Kenneth alizaliwa Novemba 1965 huko Bahati, Nairobi. Yeye ni mbunge mwenye taaluma ya masuala ya benki. Anagombea urais chini ya chama cha Kenya National Congress, pamoja na mgombea mwenza Ronald Osumba.
Kenneth Pia alidhamiria kuipa polisi vifaa na kuwalipa vizuri maofisa ili kuwahamasisha kufanya kazi nzuri, na anaamini kwamba maendeleo na elimu katika maeneo yanayokumbwa na uhalifu yatazuia vitendo haramu. Anapanga kulipia programu zake kwa kupunguza matumizi makubwa ya Serikali.
Kenneth ana shahada ya kwanza na ya uzamili katika sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi, pamoja na kozi ya shahada ya juu kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Programu ya Utendaji kwa ajili ya Maendeleo ya Usimamizi huko Lausanne, Uswizi.